Monday, June 11, 2012

KUMBUKUMBU CHUNGU!

HAPA ndipo mkulima Mwamwindi alipomuua aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa enzi hizo aliyeitwa Kleruu. Ni historia chungu lakini tamu. Inapatikana eneo la Mkungugu njiapanda ya kwenda Ikengeza, Iringa Tanzania

MTO RUAHA!

UNAVYOONEKANA katika nyakati za kiangazi. Ni moja ya mito inayovutia sana Tanzania. Mto huu una umbo la kupindapinda kama joka kubwa linalotembea. Unapatikana mkoani Iringa!

TEMBO MKUBWA ZAIDI!

ANAPATIKANA katika hifadhi ya wanyamapori ya Ruaha iliyopo mkoani Iringa.

Sunday, June 10, 2012

IGANGILONGA

Hili ni jiwe liitwalo Gangilonga. Wakazi wa asili wa Iringa (wahehe) walilipa jina jiwe hili wakiwa na maana jiwe linalosema. Hii ni kutokana na mwangwi unaotokea unapozungumza kwa sauti kubwa katika eneo hili!

ISIMILA

Hapa ni kwenye hifadhi ya mambo ya kale, Isimila Iringa. Hifadhi hii ina miaka mingi na ni ya kipekee zaidi duniani!

FAHARI-TANZANIA!

HII NI BLOG ITAKAYOJIHUSISHA NA MASWALA ANUAI YA VIVUTIO VYA KITALII VILIVYOPO HAPA NCHINI TANZANIA. NI BLOG ITAKAYOKUELEZEA WAPI PANA NINI NA WEWE MGENI UTAWEZA KUJIPATIA HICHO UKITAKACHO KATIKA HAZINA YA NCHI YETU.

TANZANIA TUNA UTAJIRI MKUBWA WA MBUGA, MITO, MABWAWA, BAHARI, MILIMA, TAMBARARE, MIINUKO, MABONDE, HAZINA YA UTAMADUNI, HIFADHI ZA MAMBO KALE, HISTORIA CHUNGU LAKINI ZINAZOVUTIA NA VINGINE VINGI VIZURI.

NI SEHEMU NZURI AMBAZO ZITAKUONDOLEA MSONGO WA MAWAZO NA KUIFURAHIA KAZI YA MUNGU AMBAYO KWA HAKIKA HAINA DOSARI.

NIPO IRINGA TANZANIA NA KWA MAELEZO ZAIDI IKIWEMO KUPELEKWA BAADHI YA MAENEO TUWASILIANE KWA NAMBA ZIFUATAZO


0715 439740 AU O754 439740
Email: kwetuzaidi@gmail.com

KARIBU SANA!